ZIWA NGOSI

 







Ziwa Ngosi ni kreta kubwa ya pili Africa baada ya ile ya Ethiopia.

Ngosi ina muonekano wa Bara la Africa ndio upekee wake linapatkana milima ya Upoloto Mbeya Tanzania.

Ziwa hili limetokana na mlipuko wa volkano hivyo ni tofauti na maziwa mengine. Upekee wa ziwa hili ni kwamba liko ndani ya milima ya upoloto katikati ya misitu na lina urefu wa km 2.5, upana wake ni km 1.5, kina chake ni mita 74 na lina ukubwa wa hektari 9332.














Maajabu mengine katika ziwa hili ni kwamba maji ya Ziwa Ngozi huwa lina muonekano wa rangi tofauti tofauti kila wakati, kuna wakati ukifika unakuta ziwa lina rangi ya samawati, kijani au nyeusi.  misitu husababisha rangi ya maji kubadilika.


Ziwa hili halina wanyama hai wala halina hata samaki na wataalamu wanasema si salama kwa kuogelea.













Karibu sana ziwa Ngosi karibu sana Mbeya.

VisitMbeya

Follow us through our twitter site @VisitMbeya



Comments

Popular posts from this blog

KITULO NATIONAL PARK MBEYA

MBEYA PEAK/Kilele cha Mlima Mbeya